GARLIC POTATOES

Unaweza kula na beef, fish, chicken au hata Vegies



Jinsi ya kupika viazi hivi vya Garlic

Hatua ya 1. Andaa kila kitu kwanza kuliko kuanza kukimbia kimbia wakati wa kupika

Unakata kata mbwembwe za aina tofauti katika vipande vidogo vidogo sana

Karot, Hoho za rangi rangi, Vitunguu maji na Vitunguu Thaumu vya kuponda vya kutosha



Hayo ndio mahitaji ya mwanzo



Hatua ya pili ni kuviosha viazi na kuvikata vipande vidogo vidogo kwa ukubwa wa kiazi kimoja kupita mdomoni kwa wakati mmoja



Weka maji kiasi kidogo kama kikombe kimoja na nusu, weka chumvi kisha chemsha mpaka viive wasnani bila kumomonyoka na kuanza kutoa unga unga



kisha vitoe jikoni umwage maji yoyote yaliobaki na kuviacha vikiwa vikavu



Hatua inayofuata ni kuweka Butter katika kikaango nakuikaanga kwa muda wa dakika moja



Ikianza kuyeyusha unaweka viazi pamoja na mboga mboga zote zilizokatwa, hakikisha Garlic inajitokeza zaidi maana ndio yenye kuleta ladha



Unavikaanga kwa dakika 5 -7 mpaka vichanganyike vizuri



Kisha unaweka maziwa ya maji vijiko 5 unaacha kidogo yachemkie mpaka yakauke, hii ni kwa viazi 3 vikubwa ambavyo huwa ni portion ya mtu mmoja





Ukipakua inaonekana hivi, ukila sasa ndio usiseme

Wengine hukamulia na ndimu au Limao kwa juu, kutokana na upendeleo wa ladha ya mtu mdomoni kwake



Vinapatikana pia Nyumbani Lounge



No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive