Diet" DAY 7 "Siku Hii wanaopenda kula Watafurahi"



Siku ya saba naiandika kwa Confidence kwakuwa haina milima wala mabonde emengi sana kama vipo ni vya kuvikabili.

Asubuhi usiache kufanya mazoezi hata iweje. Tembea dk,30 -45

Ukiwa na partner inaweza kuwa rahisi mkiwa mnasindikizana huku mnapiga story inasaidia kujisahau na kustukia muda umeisha.



Kama huna hata peke yako haina tatizo, maadam umeamua.

Ukirudi fanya sit ups nyingi kwa kadri ya uwezo wako



Kunywa maji ya moto/ vuguvugu Glass 4 kama kawaida

Kikombe kimoja cha Chai au kahawa,

Yai moja la kuchemsha na maziwa Glass moja



Vipi! kuna unafuu kidogo au bado sana?





Kabla ya kula Lunch: Kunywa tena maji moto/vuguvugu glass 4

Halfu unywe Vegetable Noodle Soup pamoja na ndizi moja ya kuchemsha "Bukoba"

Sio zile ndizi za sukari.



Baada ya hapo kula matunda mengi sana ya kutosha, hata ukila ndizi mbivu pia kwa leo ni sawa tu

Hii ishu hapo juu iache kwanza

Jua likizama tembea dk.30-45 ukirudi fanya sit-ups ingia bafuni kuoga



Usiku ni wakati wa BBQ, wakati unangojea huku unazungumza unakunywa maji moto/vuguvugu glass 4.



Kama utachoma BBQ nyumbani ni sawa, kama utaagiza kutoka nje pia ni sawa

Ila kwa muda ule wakati unasubiri mlo unweza kunywa hayo maji



Kwasababu kuchoma nyama sio kitu rahisi sana na sio kila mtu anajua







Siku ya 7 unatakiwa kula nusu kuku kwenye Dinner yako, ila sio lazima umalize

"Hiyo mishkaki haipo kwenye diet, usiihesabu"





Unatakiwa pia ule Salady ya aina yoyote ile kwa wingi wowote ule









Ususahau kuomba dua pia kabla hujala



Leo ni wali maharage, Nusu kuku au "Beef Sausage" na salady kwa Dinner



Unaruhusiwa kunywa glass 2 za white wine baada au wakati unakula kama ni KUKU

Au glass 2 za redwine baada au wakati unakula kama ni Beef Sausage

Ila kama ni Kuku iwe Kuku

Kama ni Beef sausage iwe hiyo na sio vyote viwili



Kwa hii siku ya 7



Wine mwisho ni glass 2 tu

Manake ukifanya komeshea ukalewa kesho yake utashindwa kuamka asubuhi na hutaweza kuendelea na diet kwakuwa.



Kwanza unaweza kuwa na hang over itakayokupelekea uanze kutafuta vyakula vingine tofauti na mtiririko wa hatua hii tunayopitia.

Pia ukichelewa kuamka hutoweza kufanya mazoezi na uta skip moja ya mlo wa siku



Jiandae ya siku ya 8 ni ngumu zaidi, baada ya kuji spoil na week end



No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive