COASTAL UNION YAPATA MSAADA





.



KLABU ya Coastal Union ya Jijini hapa imepokea msaada wa vifaa vya

michezo vyenye thamani y ash 2 milioni kutoka kwa mdau wa michezo

nchini Mohamed Bawazir ikiwa ni mchango wake wa kuiwezesha kushiriki

vyema ligi kuu vodacom.



Vifaa hivyo ni jezi,mipira,beeps soks jezi za walinda mlango kwa ajili

ya wachezaji pamoja na vifaa vya uhamasishaji vya kutumiwa na

mashabiki ambavyo ni vuvuzela na tambara la hamasa.



Makabidhiano ya vifaa hivyo yalifanyika jana asubuhi katika hoteli ya

Tanga Beach Resort ambapo clabu ya Coastal iliwakilishwa wapenzi wake

wakiongozwa na Mwenyekiti wao,Ahmed Aurora na Makamu mwenyekiti

Steven Mguto.



Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo,Bawazir alisema lengo ni

kutoa hamasa kwa wadau wengine kujitolea kuisaidia Coastal Union

inayokabiliwa na michuano ya Ligi kuu Vodacom pamoja na kuendeleza

michezo kwa ujumla katika mkoa wa Tanga.



“Nimeamua kuongoza njia ili wadau wengine wajitokeze kusaidia kuhuisha

michezo katika mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa ikiwika katika miaka ya

nyuma kwenye michezo mbalimbali”alisema Bawazir.



Mdau huyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Darworld Links Ltd ya

jijini Dar es salaam,alisema kuna kila haja kwa wadau wa Tanga walioko

maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi kujitokeza kusaidia.



Vifaa vilivyokabidhiwa ni sare jozi moja,seti mbili za sare za walinda

mlango ,soks pea 20,jezi za mazoezi jozi 30,mipira mitatu aina ya

jabulani,bendera na tambara kubwa la hamasa.



Mwenyekiti wa klabu hiyo,Aurora alimshukuru mdau huyo kwa mchango wake

mkubwa ambapo alisema vifaa hivyo vitawasaidia wachezaji pamoja

mashabiki wakati wa michuano yote inayoikabili timu hiyo.



“Bawazir amekuwa mdau wa kwanza kuisaidia klabu yetu ukiacha wadhamini

wakuu,tangu tumechaguliwa tumekuta Coastal haina vifaa wala chochote





No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive