KITENDO KILICHONITOKEA AIRPORT YA MUNICH - GERMAN NI STORY YA SIKU

Nilishuka Airport ya Munich nikitokea Amsterdam ili kuunganisha ndege ya kwenda Greece Katika hiyo ndege mimi tu ndio nilikuwa wa rangi ya giza wengine wote walikuwa wang'avu wa ngozi.

Nikaingia toilet ili kujiweka sawa kabla ya kurudi kuchukua boarding pass kwenye machine zilizoko airport nikaskia naguswa bega. Wanaume wawili walikuwa wamevaa nguo za kiraia waliomba kuona Tiketi na Boarding pass yangu, kwanza nilidhani inaweza kuwa ni wezi tu nikakataa

Nikawauliza nyie mnataka kuona Tiketi yangu ya kazi gani huku nikijaribu kuondoka kwa kuwapuuzia, wakanizuia njia. Wakasisitiza, nikamuuliza tena mmoja wao..

Kwani wewe ni nani hasa??
Akafunua koti lake upande wa kiunoni akanionesha short Gun Nilipostuka kiaina akatoa ID na kunifahamisha kuwa yeye ni Police Officer

Ikabidi niwe mpole, nikachukuliwa nikaingizwa kwenye kachumba flani hivi
Nikapekuliwa humo weeeeeeeee, Maswali kibao Eti mbona Passport yangu ina mihuri mingi sana, na kuwa nina fanya shughuli gani

Naonekana kama wa kubeba mzigo?? Hata sielewi Baada ya kukosa walichotafuta wakaniachia niende nikiwa nimetumbukiwa nyongo kwa hasira

Ila wenye ngozi ng'avu hakuitwa hata mmoja, nili mind sana Hii ilinitokea Bergen - Norway Airpot pia japo huko sikuonyeshwa ka bastola
Hizi picha ni mfano tu wa vitu nilivyoonyeshwa na askari hao walionipekua pekua

No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive