20 July Machozi ilipiga Maisha club,Huko Hamnaga Picha, IJUMAA 22 JULY 2011. CHOZI LIKALIA TENA NYUMBANI

Kama masihara, lakini ni kweli MACHOZI BAND sasa imefikisha miaka 6 tangu kuanzishwa na Ijumaa ya tar 22 tuliamua kufanya pary ya kusherehekea ushindi na mafanikio yetu ambayo yanaweza kuwa ni kidogo kwa wengine lakini hatua kubwa sana kwetu.


Kutambua na kuthamini mchango wa wanamuziki na wadau waliokuwa na sisi tangu tunaanza hadi leo, tuliamua kutoa Tuzo kuwashukuru kwa mchango wao.

Pichani juu Ni Mwinyi Goha, akikabidhiwa tuzo ya Mwanamuziki anejipenda na mwenye muonekano Safi, kuanzia mavazi n.k kwa kipindi chote ambacho yupo kazini.
Swahiba, Shamim Mwasha akimkabidhi Mbwana Mponda Tuzo ya Mwanamuziki aliekaa na Band kwa muda mrefu kuliko wengine wote.
Huyu anapiga Bass Guitar, Tangu MACHOZI inaanza mpaka leo yupo

Jonico Flower, Best Vocalist hilo halipingiki hata Jide anaweza kusubiri hapa

Mfanyakazi Bora alikuwepo lakini alikuwa kazini hakuweza kuinuka hata kuifuata Trophy yake, mkewe akamchukulia akampelekea pale alipokuwa amekaa
Huyu si mwenye Tuzo, ni mke wa mwenye Tuzo hiyo inayoonekana pichani juu

Baada ya kupokea kikombe na bahasha ya fedha taslimu alienda kuzikabidhi kwa baba kwanza, zikatiwa barka halafu kama ma mwenye nyumba akarudi nazo kuzimiliki na kuzipangia budget
Mfanyakazi bora wa MACHOZI BAND anaitwa DUDU
Best Male Supporter "ERASTO LUGENGE"
Pamoja na kuwa tunaimba watu wanakuja, lakini kuna watu huwa wanakuja kila siku, lije jua ije mvua na tumetambua mchango wao.

Best Female Supporter "TINDWA"
Tangu Chozi linaanza JJ Blue mpaka linapata makazi yake Nyumbani,
mdau yupo tu



Mwanamuziki mwenye nidhamu zaidi anaitwa Jules


Hiii nitailezea juu



Tanzania kuna wanawake wazuriiiiiiiii, sana, so natural

Picha ziko nyingi, Tuzo ziliendelea mpaka Jumapili kwa abao hawakuwepo Ijumaa kuchukua Vikombe vya, tunalala kidogo kwakuwa muda umeenda.
Tukiamka tutawapa picha zaidi hii ni TRELA, Mkanda kamili waja

No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive