MAPISHI YA NSANSA TOKA TABORA

Unaziloweka kwenye maji zaidi ya robo saa ili mchanga uweze kutuama kwakuwa huwa una michanga midogo midogo

Unauosha huku unaupikicha kuhakikisha mchanga unatuama, waweza uosha zaidi yamara tatu uwe msafi zaidi.

Haya ni majano ya kunde yaliyochemshwa yakakaushwa.Baada ya kukauka wamechanganya na uyoga uitwao KANSWELELE ni mdogo mdogo sana

Unakaanga vitunguu na nyaya, vikiiva na kulainika unaweka mboga yako uliyoosha unageuza geuza unaweka chumvi, unaifunika baada

Unaweka Karanaga zilizosiginwa, unakuwa unaugeuza geuza ili zisishike kwenye sufuria.
Ukiridhika kuwa karanga zimeiva unaipua

Unakula na chakula kama Ugali, Wali na Mihogo au Viazi

No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive