DIET SIKU YA 15 -21, Round ya 3.........


Hii wiki inaweza kuwa ni rahisi sana au inaweza kuwa ngumu kutegemea na utakavyoichukulia
Chagua mlo mmoja tu mzito kwa siku, muda mwingine jazia jazia tu
Sio lazima ule asubuhi mchana jioni

Maji na matunda ni vitu vinavoweza kuchukua nafasi kubwa katika tumbo lako na kufanya usisikie njaa na kutamani kula mara kwa mara.
Kama unajua kuogelea unashauriwa kufanya hivyo dakika 20 -30 angalau mara moja kwa wiki
Ukitaka muscles zi function vizuri kunywa atleast maji litres 2 kwa siku kama unafanya mazoezi

Kama hufanyi mazoezi kutegemeana na afya yakounaweza kunywa 1.5litres kutegemeana
Jitahidi kuepuka maji baridi, kunywa maji kawaida au ya uvugu vugu.

Day 14 - 21


Hazitofautiani sana
Unatakiwa kuchagua simple breakfast ya mfano huu

Break fast Choice ya 1:

2 Slices of toasted brown bread
1 small banana
1 boiled egg
1 glass of orange juice
1 Kiwi fruit
ofcourse unaweza kunywa na Coffee au Tea yenye kijiko kimoja tu cha sukari

Break fast Choice ya 2:

Cornflakes na maziwa ambayo ni skim
Matunda yaliokaushwa "Dried fruits"
1 fried egg

Unaweza kuongezea vitu kama yoghurt katika breakfast yako

Light Lunch:


Inashauriwa kula chakula ambacho kuna matunda na mboga zenye rangi mbali mbali, inaaminika kila rangi ya chakula ina umuhimu wake katika mwili.
Mbali na kuvutia kwa sura.

Katika kuchagua unaweza kula vitu light kama:

Roasted beef
Boiled Chicken
Grilled fish

na katika kila mlo unaweza kuambatanisha na Coocked vegetable, toasted bread kama slice 2 hivi zinatosha, rice 1 cup au boiled banana (bukoba)
Ni muhimu pia kula matunda kiasi

Unaweza kubadili kwa jinsi unavyopenda huku ukizingatia kuweka kiasi kidogo sana cha chakula kwenye sahani yako.
Ukiweza kuepuka red meat pia ni jambo la busara zaidi




Dinner:


Salad inatakiwa kwa wingi sana kila usiku
Itengenezwe kwa kuweka vitu mbalimbali vyenye rangi tofauti
Kama nyanya, vitunguu, letuce, olives (black or green) hoho za rangi tofauti n.k

Kula vitu light kama:

Chicken stir fry with noodles
Supu ya samaki/ Kuku
Mishkaki

Bila kula wanga kama Ugali, Viazi (Chips) au Wali nyakati za usiku

Katika kila mlo zingatia kunywa maji moto
Fanya mazoezi angalau mara 3 kwa wiki, likiwemo zoezi la kikubwa

Picha halisi za humo ndani kumefikia hali gani tukiumaliza mwezi wa pili.

Mazoezi unayotakiwa kufanya katika mlolongo huu ni:

Kuruka kamba dakika 20 -30 "mara 3 -4" kwa wiki
Sit ups 100 - 150
Kutembea au kukimbia kama hutaweza kuruka kamba.
Kuogelea angalau mara moja kwa wiki
Na kushiriki katika tendo la ndoa mara 3-4 kwa wiki

No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive