Ni bora kuliko kuja mjini?
Ila naona sivyo, labda ndio maana kila mtu anakimbilia mjini
Ila ingekuwa poa kama kungekuwa na elimu na mambo kama ya mjini katika mazingira haya halafu hao wanaoishi huku wapajenge kwao pawe kama mjini ili wasikimbilie mijini
Hakuna joto kama mjini, Ni baiskeli tu tena wala sio nyi nyingi kama magari ya mjini
Ajali si mara kwa mara labda iwe ya kuumwa na nyoka shambani au kuanguka toka juu ya mti
Au kutumbukia kisimani wakati unateka maji
Huhitaji steelwire kusugulia hizo sufuria zinazoonekana zinang'aa hapo juu
Unahitaji mchanga laini tu ambao huundwa kama kichuguu na wadudu wanaojenga maskani yao pembezoni mwa nyumba wanaojulikana kama Fukufuku
Hapo kilichogharimu ni hayo masufuria tu
Ila hiyo miti iliotumika kutengenezea chaga ni bure
Sio hatari kulala kwenye nyumba ambayo haina madirisha madhubuti kwa kijijini
Huu ni mwanzo wa story ambayo ukipenda unaruhusiwa kuifuatilia, tukijaaliwa uhai mwisho wake utakuwa mzuri.......Ni story ya kujenga.
Pnapomajaaliwa tukutane ukurasa wa pili
Picha zote kwa hisani ya:
Captain G. Habash
Alietembelea Bunda mwezi July
No comments:
Post a Comment