MZALENDO PUB IJUMAA YA LEO........TUNAENDELEA KUTOA NAFASI KWA WASCHANA WAPYA MACHOZI BAND

Leo tunamtambulisha rasmi muimbaji mpya wa kike ndani ya MACHOZI BAND.........Huyu mtoto anaitwa Bella, anauwezo wa sauti, mvuto anao na ana confidence ya kulimiliki jukwaa.

Bella alipiga simu baada ya kusikia kuwa Machozi Band inatoa nafasi zaidi kwa waimbaji wa kike msimu huu.
Akafika mazoezini kujaribu ili kuona uwezo wake, kila mtu alimpokea na kukubali kuwa ataweza.. Kadri siku zitakavyoenda tunaamini ana nafasi ya kuwa mkali zaidi.

Na leo ndani ya MZALENDO PUB tunamjaribu Bella mbele yenu, tunawaalika mje kushuhudia muonekano mpya wa Machozi Band unaopambwa na Flowers zaidi.
Mliliulizia, tunalitimiza............

Binti wa pili kuingia katika majaribio ya kujiunga na Machozi Band alikuwa CAROL.
Bado tunakaribisha maoni yenu ili kuboresha zaidi Band yenu ya MACHOZI

KOKOYE ndio alikuwa wa kwanza kufungua milango kwa msimu huu mpya wa MACHOZI Band yenye nafasi kwa Flowers zaidi, kama ambavyo maswali mengi yalikuwa yanakuja.
Kwanini Band ina wanaume tu????????????????

LADY JAYDEE na MACHOZI BAND Ijumaa hii na zingine zote ndani ya Mzalendo Pub kuanzia saa 3 kamili Usiku.
Karibuni mu enjoy ladha mpya za sauti

KILA ALHAMIS MACHOZI BAND KAMA BAND INAYOJITEGEMEA, IPO SAVANNAH LOUNGE
JUMAPILI MACHOZI BAND IPO SWEET EAZY...

NA IJUMAA TU NDIO LADY JAYDEE KWA PAMOJA NA MACHOZI BAND


No comments:

Post a Comment

Popular Posts

Popular Posts

Followers

Search This Blog

Blog Archive